ALIKIBA: Nawaomba watu wasinikosanishe na Diamond, Sina ugomvi naye!

Alikiba anataka watu wafahamu kuwa hana na tatizo na Diamond Platnumz na amewataka watu waache kuwakosanisha.

 AliKiba amewataka watu kuachana na tabia ya kuwagombanisha Diamond ili wafanye muziki mzuri.

“Kila mtu anaandika anachotaka juu ya mimi na Diamond, mpaka wengine
wanatumia akaunti fake za Facebook kutukosanisha, ndio maana nikasema
kuna wengine wanafanya for fun na wengine wanafanya ili kutukosanisha
wengine wanafanya lakini hawajui wanachofanya,” amesema Alikiba.


“Mimi najaribu kuwaomba wadau mbalimbali waache hiyo tabia ya
kutukosanisha kwa sababu mimi sina ugomvi na Diamond na wala sina mambo
hayo. Ninachowataka waendelee kusupport kazi zetu ili mambo yaende
vizuri kwa sababu sisi ndo wasanii wao tunaoiwakilisha Tanzania.
Wanapotupa moyo wao sisi tunazidi kukaza buti ili tufike mbali zaidi.
Watu wanaotengeneza ugomvi wangu na Diamond waache cha zaidi wafanye
kusupport muziki na watuambie ni mapungufu gani ambayo yamepungua ili
tujirekebishe,” ameongeza.


Katika hatua nyingine, Alikiba amezungumzia mapokezi ya wimbo Mwana na Kimasomaso pamoja na ujio wa video zake.

“Kwanza watu wamenipokea vizuri sana kama nilivyokuwa nikitarajia,
imeonyesha ni jinsi gani yale malalamiko ya maana walikuwa wakilalamika
kwamba nimekumiss na nilivyotoa nyimbo watu wanasikiliza na kuinjoy na
nyimbo zenyewe zimekuja wakati mzuri na zenye maadili mazuri ya
kuelimisha na kuchezeka na ya kufurahisha. Maandalizi ya video yapo
tayari na booking ipo tayari vilevile, maandalizi nimeandaa hata kabla
sijatoa nyimbo, video itafanyika nje na moja ni hapa siwezi sema ni nchi
gani bado ni mapema nitasema baadae nikishaitoa, kwasababu nimetoa
track mbili moja itafanyika hapa na nyingine itafanyika nje.”

crdt:bongo5

ad

One thought on “ALIKIBA: Nawaomba watu wasinikosanishe na Diamond, Sina ugomvi naye!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *