Tuzo Za Watu 2015 Yazinduliwa Leo

Mhariri mkuu wa Bongo5  Bw. Fredrick Bundara akiwa pamoja na mwariri
msaidizi, Sandu George wakizungumza leo na waandishi wa habari katika
uzinduzi wa Tuzo za watu 2015

Tuzo za watu zaja kivingine, vipengele vyaongezeka

Kampuni ya Bongo5 Media Group, imezindua msimu mpya na wa pili wa Tuzo

za Watu Tanzania zilizoanzishwa mwaka jana ili kuwatuza watu kwenye sekta

ya burudani na habari wanaofanya vizuri.

Akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari leo, mhariri mkuu

wa mtandao wa Bongo5, Fredrick Bundala amesema tuzo za mwaka huu

zimeboreshwa zaidi kwa kuongeza vipengele vitatu vipya.

“Mwaka huu tuzo zimeongezewa nguvu zaidi. Kutoka vipengele 11

tulivyokuwa navyo mwaka jana hadi vipengele 1. Mwaka huu tumeongeza

vipengele vitatu muhimu,” amesema Bundala.

Amevitaja vipengele vilivyoongezeka kuwa ni pamoja na muongozaji

wa filamu anayependwa, tovuti/blogu inayopendwa na mfadhili maarufu

anayependwa.

“Kwenye jamii yetu kuna watu maarufu ambao wamekuwa mstari wa mbele

kusaidia jamii hususan watu wasio na uwezo ama wanaoshi katika mazingira

magumu. Tumeona ni muhimu pia kuwatambua watu hawa ambao huamua

kujinyima na kugawana kile wanachokipata ili kuwasaidia watu wanaohitaji

msaada,” ameongeza.

Amesema zoezi la kuanza kupendekeza majina ya washiriki limeanza rasmi

Alhamis hii ambapo wananchi wanaweza kuwapendekeza kupitia website ya

www.tuzozetu.com ama kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu kwa kuandika neno

TZW, code ya kila kipengele na jina la anayependekezwa kwenda 15678.

“Baada ya wiki tatu kuanzia leo tutatangaza majina ya washiriki watano

waliochaguliwa kuingia kwenye awamu ya kwanza ya mchujo ambapo katika

kipindi cha wiki mbili itafanyika michujo mingine miwili ili kuwapata washiriki

watatu watakaoingia fainali,” amesisitiza Bundala.

“Washiriki watatu kwenye kila kipengele watahudhuria kilele cha tuzo hizo

kitakachofanyika katikati ya mwezi wa tano.”

Kwa upande wake mhariri msaidizi wa Bongo5, Sandu Mpanda, amesema

kuwa utofauti wa tuzo za watu na tuzo zingine ni kuwa wananchi wana nguvu

ya asilimia 100 kumchagua mshindi.

“Kura za wananchi ndizo zitakazompata mshindi. Ni muhimu wananchi

kuwapigia kura watu wanaowapenda ili kuhakikisha wanashinda vipengele

walivyotajwa kuwania,” amesema Mpanda.

Mpanda amevitaja vipengele vinavyowaniwa kwenye tuzo za mwaka huu

kuwa ni pamoja na Mtangazaji wa redio anayependwa (TZW1), Kipindi

cha redio kinachopendwa (TZW2), Mtangazaji wa kipindi cha runinga

anayependwa (TZW3), Kipindi cha runinga kinachopendwa (TZW4), Tovuti/

Blogu inayopendwa (TZW5) na Muongozaji wa video za Muziki anayependwa

(TZW6).

Vingine ni Muongozaji filamu anayependwa (TZW7), Mwigizaji wa

kike anayependwa (TZW8), Mwigizaji wa kiume anayependwa (TZW9),

Mwanamuziki wa kike anayependwa (TZW10), Mwanamuziki wa kiume

anayependwa (TZW11), Filamu inayopendwa (TZW12), Video ya Muziki

inayopendwa (TZW13) na Mfadhili maarufu (TZW14).

Hashtag za kwenye mitandao ya kijamii mwaka huu ni #TZW2015 na

#TuzozaWatu.




Twitter: @djmwanga     
Instagram: @djmwanga     
Facebook Fans Page: DJMwanga

ad

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *