HUU NDIO USHAURI WA ALI KIBA KWA WASANII WA SINGELI

Msanii wa Bongo Fleva Ali kiba hivi karibuni alikuwa anajibu maswali aliyoulizwa na mashabiki wake kwenye mtandao wa Twitter, na moja ya maswali
hayo aliyo ulizwa ni Nini msimamo wake kuhusu Muziki wa singeli kuua Bongo fleva?

Ali kiba alianza kwa kukataa kwa kusema sio kweli muziki wa Singeli hauwezi kuua muziki wa Bongo fleva,na akaenda mbali zaidi kwa kutoa ushauri kwa wasanii wa singeli kutumia lugha nzuri na yenye staha kwani muziki wao umetokea kupendwa na watu wakubwa.

Ali Kiba

“Napenda sana Muziki wa Singeli, naaaaa endapo nitaufanya muziki wa singeli nitatumia lugha ya kistaarabu sana, yeaaa sisemi kwamba lugha ambayo wanaitumia sio ya kistaarabu ? aaaaaahhh
namaanisha kuwe na staha kidogo kwenye lugha inayotumika katika singeli, Naupenda sana muziki wa Singeli na sasa hivi umepata sapoti kubwa sana, kwa kila rika kwa sababu watu wana understand muziki yaani muziki yaani muziki hauna ujanja utaupenda tuu”
alisikika akijibu swali hilo aliloulizwa na shabiki yake.

Hakuishia hapo aliendelea kujibu swali hilo kwa kusema “Mama yangu mimi anapenda sana muziki na katika muziki anaoupenda Singeli pia anaupenda, lakini kuna lugha ambazo zinatumika kwenye singeli, mama yangu hawezi kutumia, ili muziki wao uweze kukua zaidi kwani unapendwa sana”

ad

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *